Historia

 
Historia ya ugunduzi wa bara la Amerika

.Anajulikana kama Christopher Columbus ni mzaliwa wa Spain kazaliwa mwaka 1451 na

kufariki 1504/6 akiwa na umri wa miaka 53 ni baharia maarufu sana katika historia na

wanafunzi wengi wanamtambia Chris kama mgunduzi wabara la American lakini Bado

hawaijui mpaka Leo ilikuwaje akagundua safari yake ilikuaje na yapi aliyo pitia kipindi yupo

njiani Leo tutayaona yotee . Ikumbukwe katika kipindi chote Hawa maabaria wanasafiri baharini hakukua na teknolojia

kama Leo walikuwa wakitumia merikebu (Mashua) ambazo zilikuwa zikiongozwa na upepo

tuu hivyo ili kuwa bahari ni lazima ujue majira ya mwaka vizuri na uelekea wa upepo ili

kuepukana na dhoruba wakati wasafari baharini. Napia Karne ya 15 kurudi nyuma watu wengi wa Ulaya, Afrika Amerika hakuna aliejua habari

kumuhusu mwenzie mpaka pale ubunifu wa vyombo vya majini ulipo gunduliwa , wapo

wanaosema wareno ndio Taifa la kwanza kugundua vyombo hivi vya majini . Na katika kipindi hiki chote habari zilizo kuwa zinajulikana ilikuwa ni uhindi ambapo

wafanya biashara walio wafanya biashara kati ya Ulaya na India walisimulia namna India ilivyo

tajiri na namna mfalme wa India anavyoishi anakula kwenye vyombo vya dhahabu, amevalia

mavazi ya dhahabu Pete na mapambo mengine mengi ya dhahabu . Basi hizo habari zilikuwa zina mtamanisha Kila mtuu atamani kufika huko India aonane na

huyo mfalme , kumbuka Ulaya katika kipindi hicho Cha Karne ya 15th walikuwa wapo kwenye

phase ya Bullion yaani kilikuwa na uhitaji mkubwa wa madini ya dhahabu, Shaba na fedha na

hiyo yote ni kutokana na walikuwa katika kipindi kutumia fedha kama njia ya biashara hivyo

walishatoka kwenye Barter trade system . Mfanyabiashara ambaye alijiingiza kwenye Hii

biashara ya kutafta haya madini alitajirika sana na hata ufalme ulitajirika pia. Basi bwana Chris na yeye alitamani sana kwenda huko na ikumbwe muda wote ule ulayala

hakuna aliye amini Dunia ni duara Kwani . Hivyo hakuna aliye amini ukipita njia kupika

magharibi unaweza fika India . Kwani kipindi hicho Ulaya ya kati kulitokea homa Kali ya Black death na kilikuwa na vita kati

ya waislamu na wakristu na vita hivyo vilidhaminiwa na papa yote haya yalifanya kuwe na

ugumu wa kufika huko India

Na Kwa kipindi hicho Nchi ya Ureno na Spain ndizo zilizo kuwa zimeendelea kiteknolojia

hasa za usafiri wa majini hivyo kulikuwa na ushindani baina ya nchi hizo mbili kwamba anaye

kuwa wakwanza kugundua maeneo mapya bas anaweka bendera yake na kutangaza kuwani

eneo lake na upaswi kumwingilia . Basi kilicho tokea ni Mfalme wa Spain na Ureno kutoa udhamini Kwa yeyote ataye weza

kutafta njia ya mpya ya kufika India Kwa upande wa Ureno ntaelezea siku nyingine Leo tupo

Spain. Basi mnamo mwaka 1492 August Mfalme alimpatia Columbus meli ndogo tatu na hapo

ndipo safari ilipo Anza kutoka bandari ya Spain iitwayo Palos . Zile meli Chris alizipa majina ya

kwake aliita Sanat maria akimaanisha maria mtakatifu na Zile mbili ziliitwa pinta na Nina. Kumbuka kabla ya safari Chris alionekana mwenda wazimu mabaharia wengi waliogopa

kusafiri naye hivyo Kwani hawakuamini kama safari inawezekana , basi siku tatu baadae meli

iitwayo pinta ilionekana usukani wake umelegea lakini ukweli ilikuwa mabaharia wawili lengo

ni safari ihairishwe na Chris arud nyumbani . Siku mbili baadae nahodha wa pinta

aliutengeneza lakini siku chache baadae uliharibika Tena hivyo Chris alilazimika kutia nanga

katika visiwa vya Canary ambavyo ni Mali ya Spain hivyo walitia nanga ili waweke usukani

mpya na ilitumika wiki tatu kukamilika Kwa usukani huo. Na usukuni ulikamilika na safariSasa hapo ndo ilikuwa safiri imeanza rasmi kwenye bahari isiyo julikana Kwanini waliita

hivyo kwasababu hakuna aliye wahi safiri kupitia uelekeo huo . Chris alihesabu maili na mail

pasipo kuwajulisha watu wake . Siku Moja wakati wapo njiani Kulikuwa na maradi sana lilipiga

Radio Kali kiasi kwamba mabaharia waoga walisemaa ni ishara ya wao warudi nyumbani

lakini Chris aliamuru wasonge mbele lakini siku kadhaa mbelen bahari ilikuwa shwari na meli

ilikuwa ikienda vizuri tuu pasipo shida Chris alifurahi sana Kwani watu walikuwa hawaaamini

kama Kuna upepo uvumao kupelekea Spain hivyo meli zilikuwa zikienda bila wasi wasi Wala

kugeuza matanga . Inakadiriwa kuwa ni majuma matatu tangu watoke kisiwa Cha canari ndipo asubuhi jua

lilipo chwaa nahodha wa pinta meli iliyo tangulia mbele alipaza sauti kuwa anaweza kuono

nchi kavu Kwa mbali . Chris kusikia hivyo alipiga magoti kumshukuru Mungu labda kwakuwa Chris alikuwa mtu

wa Mungu ndo maana alikuanaamini kuwa anaweza kufika na pia kulipa jina meli yake sanata

maria ni ishara Chris ni mcha Mungu , Kwa upande wa Nina Wao walipanda juu ya mlingoti

kujihakikishia nao pia waliweza sema wanaona nchi kavu . Basi kilicho fwata Chris aliamuru meli zote tatu zielekee upande ule wa nchi kavu usiku

kucha kulipo kucha jua lilipo toka chaajabu hawakuona kisiwa walichoona ni bahari tuu

kumbe Yale waliona ni mawingu ndio yaliwadanganya . Kumbuka Mfalme wa Spain alihaidi kumpatia zawadi yeyote atayekuwa wakwanza kuona

nchi kavu hivyo ilikuwa ni kama mchezo wa maahindano meli ya Nina ndiyo iliyo kuwa mbele

ya msafara hivyo mabaharia wake walikuwa na matumain kupata tuzo hiyo ya mfalme . Basi

siku chache baadae meli ya Nina ilipiga mzinga kuasharia Kuna kisiwa mbele lakini haikuwa

kweli macho yaliwadanganya . Naweza kusema hamu waliyo kuwa nayo ya kutaka kuwa

wakwanza kuona nchi kavu ndo iliyo wasababisha waone Kila kitu ni nchi kavu kumbe

mawingu. Wale mabaharia walighairi na kukata tamaa ya kupendelea na safari. Lakini Chris

aliwapamoyo na kumtanguliza Mungu mbele . Asubuhi yake walipo amka waliona ndege aina ya vitwitwi na kuangalia baharini vizuri

waliona Jani hivyo niishara kuwa kisiwa hakipo mbali ilipo fika saa nane usisu Chris aliona

kwambali aliona kitu kama mwanga unawaka na kuazima mwanga kama wa mshumaa ndipo

alipo amuru meli zote zisimame na kungja Hadi kesho palipo kucha waliona Mchanga wa

bahari 😳 ilikuwa mshangao na furaha isiyo na kifani waliona wakati wanakarbia waliona

wenyeji wanakuja Kwa Kasi huku wakiwa wanakuja kushangaa meli na hapo ni wiki kumi

tangu walipo toka canary na Chris aliamuru kutia nanga walipo fika Cha kwanza waliweka

mlingoti wa bendera ya mfalme wa Spain kuasharia hicho ni kisiwa Cha Spain Chris alikiita

San Salvador maana yake ikiwa mwokozi mtakatifu na hiyo ni kutokana na kuwa walikuwa

washa katatamaa. Waliposhuka wenyeji walikimbiaa lakini baada ya muda walirudi na ndipo Chris akawapa

zawadi Kofia, njuga,shanga na vibumba vya Uzi wa Kamba wenyeji walifurahi sana pia

waliona kama Chris Amerika mbinguni kutokana na mavazi waliyo vaa na rangi Yao nyeupe . Ndipo Chris lipo andika kitabuni

Kuwa wenyeji hao hutembea uchi kabisa maumbo yao ni mazuri na sura zao pia ni nzuri

rangi Yao ni weusi kama wale wa visiwa vya Canary , anaendelea kuandika wengine hujipaka

rangi nyekundu wengine nyeupo wengine hujipaka mwili mzima wengine puani wengine

machoni . Wakati wapo kambini mmoja wa wale wenyeji alaishika upanga akajikata Kwani

alikuwa hajui kisu au panga kama kinaweza mkata , wanatumia mitumbwi kusafiria majini

mitumbwi hiyo inaweza kubeba Hadi watu 40 mingine midi ya mtu mmoja hutumia kifaa

kama mwiko mkubwa kuendeshea . Bahati mbaya Chris lipo watazama aliona baadhi Yao wamejichoma Pini ya dhahabu puani

na ndipo alipoona kuwa sasa amefika Kwa yele mfalme tajiri atumiaye glass ya dhahabu namakombe mengine . Kumbe yupo kwenye sehemu ya bara kubwa Lilo julikana lakini baada ya watu kupata habari

zake alikiita American ndo mpaka sasa linaitwa hivyo . Chris alikuwa na hamu sana ya kujua na kumuona mfalme huyo ambaye habari zake

amekuwaa akizisikia Kwa muda pasi kujua amegundua njia ya kwenda bara jipya lisilo

julikana ndipo alipoanza safari ya kuondoa kisiwani hapo maana alikwishwa gundua hapo

sio India Chris aligundua visiwa vingi kama Fernandina kisiwa kilicho pewa jina la mfalme wa

Spain na kisiwa Cha Isabella Kwa heshima ya malkia vingi aliviita juani jina la mtoto wa

mfalme Kisiwa hicho Cha juani sasa ndio linaitwa Cuba mpaka sasa jina lake ndo Hilo

ikumbukwe Chris wakati anaondoka aliondoka na wenyeji wa San Salvador ili wawaelekeze

njia wenyeji hao walikuwa wakiwaogopa jamii ya watu walio waita Caribs ambao wao ni

desturi Yao kula nyama za watu . Chris hakubahatika kuona dhahabu ila alikutana na viungo vya vyakula vingi pia wenyeji hao

walikuwa wakivutaa majani ambayo kwasasa yanaitwa Tumbaku . Walikaa kwa muda kidogo walilo ondoka walifika katika kisiwa Cha Haiti na ilikuwa ni siku

ya kuzaliwa yesu krismass . Alikuwa amechoka sana usiku ule ilimbidi apumzike Kwani hakulala siku mbili basi

alikwenda kulala Kwa sababu bahari ilikuwa shwari kazi ya kuongoza chombo alimwachia

mtoto usukani , ilipo fika usiku wa manane meli Ile ili kokotwa na mkondo waa maji ikakwama

mchangani . Kuona vile yule mtoto akapiga kelele Chris kusikia vile akaamka na kwenda juu

alimwamrisha nahodha wa Ile meli nyingine aikwamue Kwa kuivuta meli Ile kutoka

mchangani . Lakini chaajabu wale watu badala ya kutii amri walikimbiaa mail Moja. Ili

waokokoke walikimbiaa kuelekea upande wa meli ya Nina lakini yule nahodha aliwarudisha

kurudi ili wasaidiane kuikwamua Ile meli. Ilimpasa apakue Sheena yote iliyopo kwenye meli ili ipungue uzito na mfalme wa kisiwa kile

alipeleka watu wamsaidie kuikwamua meli Ile na kupakua Shehena ile. Sasa Columbus alikuwa na meli Moja tuu Nina hivyo ili mpasa awaache baadhi ya watu ili

arudi San Salvador na wale wenyeji ili akamuonejeshe mfalme na malkia wa Spain. Kwani meli yake isinge kwama basi asinge waacha hapo basi Columbus aliwaamuru

wajenge mnara mrefu na ngome Ile wapate usalama wapo kisiwani hapo.kabla ajaondoka

walipata chakula Cha pamoja kabla ajaondoka aliwaambia watu wake wanao baki watakuwa

watu wema kwao na kuwalinda dhidi ya adui zao Caribs ikiwa watakuja kuwashambulia . Basi

bwana akipiga mzinga mmoja juu watu walio kuwepo karibu wakainama chini. Chris akaamua

wafanye mchezo wa vita lengo ni watu wale wanaobaki pale waone wale ni marafiki zao na

hivyo walifundishwa mbinu za kujihami na Caribs . Wakati anaondoka alipita katika visiwa mbalimbali ambavyo hawakuwa kuviona hapo kabla

nakimoja wapo aliwashusha wapate kula viazi vikuu walipo shuka kumbe Kulikuwa na zaidi ya

watu 50 wamejificha katikati ya miti wakiwa na Sila Columbus na wenzake walitia nanga na

walipo fika waliomba kufanya biashara wabadilishane silaha za wenyeji na shanga lakini

wenyeji waliuza silaha mbili tuu na walikataa kuuza zaidi ya hapo ukatokea ugomvi watu wa

Chris wakamjeruh Mwenyezi wakakimbia. Chris alichukia kitendo hicho Cha kuwajeruhi

wenyeji Kwani hakupenda kugombana na wenyeji wake

Basi lakini walidha wale watakuwa ni Caribs na kama watakuwa ni wao basi watakuwa

wamewapa funzo ili wawaogope watu wa Spain , Columbus akukaa sana akafinga safari

akaanza kuondoka laki meli ya Pinta ilikuwa imeharibika kidogo mlingoti wake na

hawakuweza kuweka nanga hivyo meli ya Nina ilibidi kuwa ngoja Kila mara Kwa mara. Ilikuwa ni mwezi februari ambapo bahari ilikuwa imechafukwa meli zile naddoruba Kali Columbus aliogopa Sana aliona kama wanaenda kufaa , hivyo aliandika

waraka kwenye ngozi na kupitia nta ili usiloane na aliuweka kwenye chupa ya mtu na kuitupia

baharini ili Kwa yeyote ataye uona aweze kumtaarifu mfalme wa Spain . Hatimaye Nina ikifika visiwa vya Azores ambavyo ni chini ya imaya ya wareno na akatulia

mpaka dhoruba ilipo isha na akaanza safari upya Kwa muda wa siku mbili bahari ilikuwa

shwari lakini baada ya hapo upepo ukaanza kuvuna Tena mpaka matanga ya meli ya Nina

yaka tatuliwa vibaya dhoruba iliambatana na radi Kali , na dhoruba hiyo ilidumu ndani ya siku

Saba ndipo walipo fika nchi ya Ureno . Na alipumzika Ureno Kwa muda wa wiki Moja na kuikarabati meli yake Tena lakini Chris

anadai kuwa hajawahi kuona dhoruba Kali kama hiyo tangia aanze ubaharia wake na ni

maajabu kupona kwake ndipo alianza safari kutokea Ureno kuelekea kwao Spain Ndipo alipo

fika bandalin ya Palos alipoanza safari Spain kumbuka mwaka mzima ulikuwa umeisha. Kwa upande wa Spain Kulikuwa ni furaha sana Kila mtu alifurahia kumuona Columbus

amerejea na mfalme kusikia taarifa hizo Ali mwalika katika kasri lake akapate karamu nae

alikuwa kaja na zawadi nyingi sana Viazi, dhahabu, kasuku, mimea mingine migeni , jambo

jingine wa Spain alifurahi sana kuwaona wale wageni walio ambatana na Columbus ambao

aliwachukua kutoka huko katika visiwa alivyo pita . Kuanzia hapo watu wengi walitamani kusafiri na Columbus ili wazione nchi alizo zigundua

huko alipo toka , inadaiwa alisafiri mara tatu na aliona mambo mengi zaidi na yaajabu , lakini

SI Kila mtu ataweza furahia mafanikio Yako Kuna ambao walimwonea wivu na kumpelekea

mfalme na malkia habari za uongo . Kuna hata siku Moja walirejea na mfungwa kafungwa

minyororo mfalme na malkia wali huzunika kuona vile lakini hizo zote ni figisu za kumchafua

Chris . Tangia Chris agundue hizo nchi mpya hakuishi Tena maisha ya furaha kwasababu

watu Hawa kumpenda sababu ya wivu. Chris hakuwahi kufika India katika maisha yake yote mpaka anafariki mwaka 1504/6 lakini

aliacha mchango mkubwa wakugundua bara kubwa ambalo waliliita "new world" (Dunia mpya)

na kumbuka alifa kwenye bara Hilo kibati mbaya yeye alitamani kufika India hivyo kufika huko

alidhani yupo India ndo maaana wenyeji wake aliwaita west indies yaani uhindi wa magharibi .

Previous Post Next Post

No Thumbnail

News app yako bomba sasa unaweza idownload kwa kubonyeza batani ya download hapa ,