Gaza

Misri inalaani ukimya wa jamii ya kimataifa kuhusu ukiukaji wa sheria za kimataifa wa Israel.

Kila saa, watoto 6 na wanawake 7 wanauawa Gaza, kulingana na Mamlaka ya Palestina.

Misri imelaani vikali "kimya cha kimataifa" kuhusu ukiukaji wa sheria za kimataifa za kibinadamu unaofanywa na Israel katika maeneo ya Palestina.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Sameh Shoukry alikuwa akizungumza Alhamisiwakati wa mkutano wa kibinadamu kuhusu Gaza huko Paris. Amesema: "Kile ambacho serikali ya Israel inafanya kinapita zaidi ya haki ya kujilinda," akishutumu "dhamiri ya kimataifa."

Wakati hayo yakijiri Polisi wa Israel wawakamata viongozi wa kisiasa kabla ya maandamano ya kupinga vita mjini Nazareti.

Polisi wa Israel wamemkamata Muhammad Baraka, mkuu wa Kamati Kuu ya Ufuatiliaji, kundi linalowakilisha raia wa Israel wenye asili ya Palestina.

Baraka alikamatwa, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, katika mji wa Nazareth, wakati akielekea kushiriki maandamano ya kupinga vita dhidi ya Gaza, na kutaka kusitishwa kwa mapigano, wakati ambapo wawakilishi na wajumbe wa kamati hiyo walishutumu polisi. ya kunyamazisha sauti zinazopinga vita.

Baadaye iliripotiwa kuwa Baraka alikuwa katika idara ya uchunguzi ya Bisan.

Viongozi miongoni mwa raia wa Palestina wa Israel wamelaani kile walichokitaja kuwa "sera za kuadhibu" zilizowekwa na mamlaka juu yao kutokana na vita vya Gaza.

Chanzo BBC

Previous Post Next Post

No Thumbnail

News app yako bomba sasa unaweza idownload kwa kubonyeza batani ya download hapa ,