Kenya

Rais wa Kenya William Ruto asema niwakati sasa wakufanya maamuzi magumu.

Rais wa Kenya William Ruto amesema utawala wake umekabiliwa na hali ngumu huku ukijitahidi kutekeleza ahadi zilizotolewa kwa Wakenya.

Akihutubia Wakenya kuhusu hali ya taifa taifa katika Bunge la nchi hiyo, Bw Ruto ameitaja hali ngumu ya uchumi inayopelekea kupanda kwa garama ya maisha kama kikwazo cha utekezaji wa ahadi zake kwa Wakenya na akawataka wakaze mikanda.

Akizungumzia kuhusu garama ya maisha inayotokana na mfumuko wa bei za bidhaa Bw Ruto amesema kuwa inasababishwa na suala la usalama wa chakula.

"Gharama ya maisha sio jambo la kufikirika. Lipo katika familia zote. Mojawapo ya hatua muhimu zaidi katika kushughulikia gharama ya juu ya maisha ni mkakati wa kusaidia uzalishaji wa kilimo katika sekta mbalimbali za mazao ya chakula na biashara pamoja na minyororo ya thamani ya mifugo,” amessema Rais Ruto.

"Nimejitolea kuweka aibu ya njaa nyuma yetu mara moja na kwa wote. Tulianzisha mpango wa usajili wa wakulima na ruzuku ya mbolea nchini kote ambao umewezesha kupatikana kwa mifuko milioni 5.5 kwa wakulima kote nchini Kenya. Tumeendelea kupunguza gharama ya mbolea kutoka KSh6 500 hadi 2500‘’, aliongeza.

Akizunguzia suala la gharama ya unga wa mahindi, Bw Ruto amesema serikali yake imefanikiwa kupunguza bei ya unga wa mahindi hadi shilingi 145 kwa kilo.

Amesema serikali yake imetambua matatizo ya kiuchumiyanayotokana na sababu za nje ya nchi shinikozo za kifedhana imeanza safari ya kuyapatia suluhu.

Chanzo BBC

Previous Post Next Post

No Thumbnail

News app yako bomba sasa unaweza idownload kwa kubonyeza batani ya download hapa ,