URUSI YAONYA NATO NA WASHIRIKA WAKE KUWA INASILAHA ZA KUWEZA KUSHAMBULIA NCHI ZA MAGHARIBI.

chuwaz.com


Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonya kuwa Moscow inaweza kuzipa silaha nchi kwa nia ya kushambulia malengo katika nchi za Magharibi.

Bw Putin alitoa kauli hiyo huku akikosoa hatua ya nchi za Magharibi kuipa Ukraine silaha za masafa marefu .

Nchi kadhaa ikiwemo marekani zimeipa Ukraine ruhusa ya kushambulia malengo ndani ya Urusi.

Hatua kama hiyo inaweza kusababisha "matatizo makubwa sana," Bw Putin aliwaambia waandishi wa habari wa kigeni.

"Ikiwa mtu anadhani inawezekana kusambaza silaha kama hizo kwenye eneo la vita ili kushambulia eneo letu na kuleta matatizo kwa ajili yetu, kwa nini hatuna haki ya kusambaza silaha za hadhi kama hiyo katika maeneo ya dunia ambako kutakuwa na mashambulizi kwenye vifaa na maeneo muhimu ya nchi hizo?" Rais wa Urusi alisema.

"Hayo ni, majibu yanayoweza kuwiana. Tutafikiri juu ya hilo"

Hakutaja nchi ambazo Moscow inaweza kuzisambaza silaha.

Bw Putin aliitaja Ujerumani, ambayo hivi majuzi iliiambia Ukraine ilikuwa huru kulenga shabaha ndani ya Urusi kwa silaha za masafa marefu zilizotengenezwa na Ujerumani.

"Wanaposema kwamba kutakuwa na makombora zaidi ambayo yatalenga shabaha kwenye eneo la Urusi, hii inaharibu kabisa uhusiano wa Urusi na Ujerumani," Bw Putin alisema.

Rais wa Marekani Joe Biden ameipa Ukraine ruhusa ya kutumia silaha zilizotolewa na Marekani kushambulia maeneo ya Urusi, lakini karibu na eneo la Kharkiv pekee. Ikulu ya White House imesema Ukraine haiwezi kutumia makombora ya masafa marefu ya ATACMS katika ardhi ya Urusi.

Ukraine imetumia silaha za Marekani kushambulia ndani ya Urusi katika siku za hivi karibuni, seneta wa Marekani na afisa mmoja wa nchi za Magharibi aliliambia shirika la habari la Associated Press Jumatano.

Mapigano makali yamekuwa yakiendelea kaskazini-mashariki mwa Kharkiv tangu Urusi ilipofanya msukumo katika mpaka wa kaskazini mwa Ukraine. Kharkiv, mji wa pili wa Ukraine, uko kilomita 30 tu kutoka mpakani.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza Lord Cameron amesema ni uamuzi wa Ukraine kuamua jinsi ya kutumia silaha za Uingereza na kusisitiza kuwa ina haki ya kushambulia maeneo ya Urusi.

Ukraine inasema makombora ya Korea Kaskazini yanatumiwa ndani ya ardhi ya Ukraine, na mashirika ya kijasusi ya Magharibi yanasema Urusi imekuwa ikitumia ndege zisizo na rubani zilizotengenezwa na Iran katika mzozo huo.

Chanzo 

BBC Swahili

Previous Post Next Post

No Thumbnail

News app yako bomba sasa unaweza idownload kwa kubonyeza batani ya download hapa ,